Mambo 5 Muhimu kwa Simu ya Leo





 1. Kioo
Simu ya 2014 iwe na kioo chenye pikseli za hali ya juu, hii huleta ng’aro mzuri na pia muonekano wa video na oicha huwa ni wa kuvutia, ni matarajio kuwa simu walau ifikie piksel 400 kwa kila inchi (400 ppi), simu kadhaa zimefika na kupita kiwango hichi zikiwemo simu kama vile Samsung Galaxy S5, HTC M8 na LG G2, iPhone 5S kwa upande mwengine ina piksel  326 kwa kila inchi, pia na Galaxy Note 3 nayo ina 386 ppi. Hivyo hizi ziko chini ya kiwango 400 ppi.  Ukubwa wa kioo pia ni suala muhimu kwenye simu. Ukubwa upi ni sahihi hutegemea zaidi utashi binafsi wa mtumiaji. Sisi katika Gajetek tunaamini inchi 5 ni kioo kilicho na ukubwa wa kiasi cha kutosha kwa ajili ya kuitumia simu kwa urahisi huku kukiwa na ukubwa wa kutosha kuangalia media kama vile video za Youtube.


Kamera
Kamera ni sehemu ambayo kampuni zinazotengeneza simu zinafanya ushindani wa hali ya juu. Wengi hudhani uzuri wa kamera ni wingi wa pikseli lakini ukweli ni kwamba kamwe hilo sio sahihi. Kwa mfano ni vipi lenzi ya kamera ya simu inaweza kukusanya mwanga wakati unapiga picha katika sehemu ambayo haina mwangaza mzuri, vile vile kasi ya kamera ku-focus na hivyo kutoa picha zilizo nzuri (sharp). Nokia wamejipatia sifa nzuri kwa upande wa kamera, hata hivyo simu ambazo zimetamba kwa ubora wa kamera ni Sony Xperia Z2 na hata Samsung Galaxy S5. Na simu ambayo kamera yake sio ya kuridhisha ni HTC One M8. Sio tu ina megapikseli 4 (au kama HTC wanavyoiita Ultrapikseli) lakini mara nyingi kamera hii hupoteza uhalisi wa rangi unapopiga picha, si ajabu kwa kamera ya simu hii kajikuta una picha yenye mawingu ya pinki. 

Vile vile kuna mambo ambayo yameingizwa kwenye kamera lakini hayana umuhimu, au ni teknolojia iliyotangulia wakati, mfano ni wachache ambao tayari wana TV za 4K lakini kuna simu kadhaa kama vile Sony Xperia Z2, Samsung Galaxy S5 na Note 3 zinauwezo wa kuchukua video za 4K wakati display za simu hizo hazionyeshi kiwango cha 4K. Hivyo tunadhani hii ni ziada isiyo na faida kubwa kwa wengi miongoni mwa watumiaji. 


Vifaa 
Vifaa (accessories) ni ongezo muhimu katika simu. iPhone ni simu inayoongoza kwa kuwa na vifaa vingi mbali mbali na vyenye matumizi mazuri. Hata hivyo kifaa muhimu kabisa kwa sasa ni ama band za mazoezi za kuvaa mkononi au smartwatch. Ingawa iPhone ina watengezaji binafsi wa saa au bandi ambazo zinafanya kazi na iPhone, saa kama vile Pebble watch na band kama vile Nike Fuelband, bado Apple wana haja kubwa kutoa saa yao binafsi. Samsung kwa upande wa saa ndio kampuni inayooneka kuongoza baada ya kuwa na band moja na saa tatu mpaka sasa hivi, Band ni Smsung Gear Fit na smartwatch ni Galaxy Gear, Gear 2 na Gear 2 Neo. Ingawa bado hizi zinaonekana kuwa na upungufu,wanachoonekana Samsung kuwatangulia wengine ni kuwa saa na bad hizi zinafanya kazi za smartwatch na fitness band zote tatu. Kampuni kama vile LG na Sony zote zimeshatoa ama band au smartwatch, ingawa bado hizi zinaonekana kuwa ngeni katika medani hii. 

Nguvu ya Betri
Nguvu ya betri ndio lalamiko kubwa kwa watumiaji wa simu. Nyingi kati ya simu hazifikisha hata siku kamili bila ya kuhitaji kuchajiwa tena, na hasa kwa watumiaji wa hali ya juu (heavy users) Tunaweza kusema teknolojia ya betri za simu bado iko nyuma mno kuweza kutoa nguvu ya kutosha kwa watumiaji wa hali ya juu (heavy users) walau kuimaliza siku nzima bila ya kuchaji. Kila ya simu inavyozidi kuwa na display kubwa pamoja na pikseli nyingi basi nido kadiri simu unavyokula betri haraka. 

Simu ambao inaonekana kuwa na unafuu mkubwa ni LG G2 ambayo majaribio yameonyesha inaweza kudumu zaidi ya masaa 13 ni LG G2, simu hii ina betri yenye nguvu kaisi cha 3000 mAh, ambapo simu kama vile Samsung Galaxy S5, HTC M8 na Sony Xperia Z2 zote zina betri yenye nguvu ya 2500 mAh. Phablet zenye vioo vya hali ya juu ndio zionaonekana kufanya vibaya zaidi kwenye suala la chaja. 

Betri ya hali ya chini ni ya iPhone 5S ambayo ina mAh 1560. Pamoja na udogo huu bado betri hii haifanyi vibaya sana kulinganisha na simu nyingine kwa vile iPhone ina display ndogo yenye pikseli chache kulinganisha na simu nyingine za hali ya juu. Hata hivyo simu za mwaka 2014 zimekuja na mbinu ya kuzuia matumizi ya betri kwa mfano Samsung ina “Ultra Power Saving Mode” ambapo simu inapowekwa katika mode hii inaweza ikadumu siku kadhaa bila ya kuhitaji kuchajiwa, taarifa rasmi ya Samsung ni kuwa Betri hudumu siku 12 bila ya kuchajiwa simu inapokuwa kwenye mode hii.  Sony Xperia Z2 nayo ina “stamina mode”.

Uboreshwaji wa OS

Kila baada ya muda OS huboreshwa. Simu ambazo zinafanya vizuri kwa kuboreshwa kwa muda mferu ni iPhone, una uhakika wa simu yako kupata toleo jipya la OS kwa muda wa miaka mitatu au zaidi unapotumia iPhone. KWa upande wa simu za Android Nexus peke yake ndio hupata uboreshwaji kwa haraka na kwa miaka mingi. Simu zilizobaki kila tole jipya la Android linapotoka basi kwa huchelewa na wao kuweka kwenye simu za wateja wao lakini pia nyingi huwa hazipewi matoleo mapya ya OS baada ya miaka miwli.  

Maoni